DEAL DONE, REKODI YA DUNIA YAVUNJWA KWA KUFURU YA PESA, NEYMAR SI WA MCHEZO MCHEZO
Historia mpya imeandikwa katika ulimwengu wa soka na staa kutokea Brazil aliyekuwa anaichezea FC Barcelona ya HispaniaNeymar ambaye usiku wa August 3 2017 ameweka rekodi ya kihistoria kwa kusajiliwa kwa dau la pound milioni 199 ambazo ni zaidi ya Tsh bilioni 580.
Club ya Paris Saint Germain ya Ufaransaimeweka rekodi ya dunia kwa kumsajili Neymar kwa mkataba wa miaka mitano lakini kubwa ni dau ambalo wamemsajili nalo hajawahi kusajiliwa nalo mchezaji yoyote, dau hilo ni mara ya mbili ya dau alilosajiliwa naloGareth Bale, Pogba na Cristiano Ronaldo.
Rekodi ya uhamisho wa Neymar inatabiriwa kuwa itadumu kwa muda mrefu, Neymar sasa anaungana na wabrazil wenzake Dani Alvesna Lucas Moura wanaoitumikia PSG.
“PSG wamekuwa na mipango ambayo imenivutia kujiunga nao nimecheza misimu minne Ulaya sasa nafikiri huu ni wakati sahihi kupata changamoto mpya, kuanzia leo nitafanya kila liwezekanalo kusaidia wachezaji wenzangu na timu” >>> Neymar
No comments