MAKALA:: Jinsi ya kuepuka na kujizuia kutapika safarini

Safari ni hatua na kudhihirisha hilo leo katika Afya Simon Mayunga Official, tunakuletea njia kadhaa za kufanya pindi unapojisikia kutapika (kichefu chefu) uwapo safarini.
Kitendo cha kutapika kinaweza kumtokea mtu yoyote na hii huchangiwa na hali ya hewa inapoingiliana na utokea kwa wasafiri wa majini na nchi kavu, pia hutokea mara nyingi kwa mtu ambaye hakuwahi au hajawahi kusafiri umbali mrefu.
Ili uweze kuzuia hali hii uwapo sfarini basi huna budi kuepuka kula ovyo kabla ya kuanza safari na ndani ya safari, pia usile kula vitu vyenye sukari nyingi kwani vinaweza kuharibu koo lako kutoka na sukari kuzidi.
Vile vile unashauriwa kuweka njiti ya kiberiti mdomoni ili kuzuia kutapika, na kama hitoshi lamba ndimu kila wakati kwani inakata kichefuchefu na kutapika haraka.
Hivyo vyote vikashindikana na ukaona unahitaji kutapika basi muite muhudumu wa usafiri huo, ili akupatie mfuko wa rambo uweze kutapikie humo na ukimaliza hakikisha unafunga vizuri na kuweka sehemu husika na baada ya hapo safisha kinywa chako kwa maji safi na salama.

No comments

Theme images by hdoddema. Powered by Blogger.