JINSI YA KUDUMISHA AFYA NJEMA NA KUISHI MAISHA MAREFU







Katika hali ya kawaida, hakuna mtu ambaye ana uhakika mkubwa wa maisha yake kwamba ni lazima afike kesho. Muda na dakika yoyote ile unaweza kuachana na mwili wako na ukafa. Swala la kufika kesho au kutofika huwa mara nyingi linabaki mikononi mwa Mungu mwenyewe.


Pamoja na kwamba binadamu huyo hana uwezo wa kujua kesho yupo au hayupo, lakini upo uwezo wa kutambua kama binadamu huyo ataishi maisha marefu au mafupi. Inawezekana unaanza kujiuliza maswali hilo linawezekana vipi? Tulia usiwe na wasiwasi nitakwambia.



Kwa mujibu wa wataalamu wa afya wanadai kwamba, ikiwa binadamu ataishi maisha yake ya kawaida bila kupata  changamoto nyingine za nje yake kama kugongwa na gari au  namna yoyote ile ya kukatisha uhai wake upo uwezo wa kujua maisha yake yataishia wapi.



Wataalamu hao wanatuonyesha viashiria ambavyo vinaonyesha kama ukiishi hivyo ni lazima uishi maisha marefu. Mambo hayo au viashiria hivyo walivyotoa, ni matokeo ya utafiti yaliyofanywa hasa kwa watu walioishi miaka 100 na kuendelea.



Kwa mfano utafiti huo ulionyesha, watu wanaokula vyakula vyenye mafuta kidogo, watu hawa wao waliishi maisha ya muda mrefu. Mara nyingi ni kweli unapokula vyakula vya mafuta kidogo hiyo inakusaidia sana katika swala zima la mwili wako kutopata magonjwa  hovyo.



Pia utafiti huo uliendelea na kuonyesha kwamba, watu wanaokula vyakula vyenye wingi wa protini pia afya zao ziliimarika zaidi na kupelekea kuwa na maisha marefu. Vyakula hivyo ni kama  samaki, dagaa, maharage, nyama ana vinginevyo.



Hata hivyo pia watu wanaofanya mazoezi kila siku nao pia walionyeshwa kwamba wanauwezo wa kuishi maisha ya muda mrefu kutokana na mazoezi huweza kuimarisha afya na kupunguza baadhi ya magonjwa na hali za kunenepeana hovyo.



Hivyo utaona, vyakula visivyo na mafuta sana, vyakula vyenye protini na kufanya mazoezi ni mambo ambayo yametajwa na wataalamu yanaweza kuboresha afya yako na kupelekea kuwa na uwezekano mkubwa sana wa kuishi maisha marefu.



Kumbuka siku zote, afya ni kitu cha muhimu sana katika maisha yako na safari yako ya mafanikio kwa ujumla. Kama ukiwa huna afya njema hakuna utakachokifanikisha kwenye hii dunia. Ni muhimu sana kutunza afya yako kwa ajili ya mafanikio yako.

No comments

Theme images by hdoddema. Powered by Blogger.